ZOEZI LA BVR LAZUA KASHESHE KWA WAANDIKISHAJI GEITA



Geita: Wananchi wa Mtaa wa Buhalahala ,kisesa na Moringe  wamewafungia ndani waandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura na kupiga mawe gari za serikali kisha kuvunja vioo vya nyuma  kwa  kile kinachoelezwa kuwa muda wa kuandikishwa umekwishana wao hawajaandikishwa.

Wananchi hao waliamua kuchukua maamuzi hayo kutokana  kuhofia kutokuandikishwa na kukosa haki yao ya msingi ya kupata kitambulisho kitakachowawezesha kumchangua kiongozi wamtakae na pia kitambulisho hicho kuwasaidia katika mabo mbalimbali ikiwamo kusafiri na matibabu.

Zoezi hilo ambalo lilianza 17 Juni mwaka huu kwa kata tatu ambazo ni Buhalahala,Mwatulole na Kalangalala za mjini Geita na kumalizika  23 Juni mwaka huu(Jana)  ilizua taflani katika vituo hivyo ambapo wananchi walikaa kituoni hadi usiku huku wakizuhia waandikishaji wasiondoke kituoni mpaka wananchi wote waandikishwe.

“Mimi nimekuja hapa nina siku ya tano leo kila nikija sipati nafasi ya kuandikishwa,wanaadikisha watu wenye pesa zao sisi maskini tunabaki kuangalia tu,wengine wanalala wanakesha vituoni siku ya tano lakini hawajaandikishwa na leo ndiyo mwisho”alilalamika Marwa Ernest mkazi wa mwatulole.

“Tumemzuhia huyo anayeandikisha hasitoke ndani mpaka atuandike wote tuliopo hapa ,hatuogopi cha polisi wala cha nani kama nikutua watatuulia hapa ,tunachotaka ni haki yetu ya kuandikishwa ,cha kushangaza wanaacha kutuandikisha wazawa wa eneo hili wanandikisha watu wanaotoka kata zingine hiyo ni haki kweli?”alihoji  Neema Charles.

Charles aliongeza,”chakushangaza mwandikishaji anatuambia macho hayaoni ,kwa hiyo sisi tufanyeje, tunataka kitambulisho kwani ndiyo cha msingi mwaka huu”alilalamika.

Wananchi hao ambao walionekana kuwa na jazba huku wakitishia kuchoma mashine kama hawataandikishwa  walisikika wakisema kuwa zoezi hilo lilijaa ufisadi kwani watu wengine wenye pesa waliandikishwa kwa njia ya simu yaani watu walituma taarifa zao kwa simu na kuandikishwa.

“Msiachie wazi huko baneni  mlango,kazeni uzi huko msimpe nafasi ya kupita mpaka tujue muafaka wetu haiwezekani watu tunakuja kila siku hapa tukifika tunaambiwa tuandike majina lakini hatupewi vitambulisho ,hapa hatoki mtu ...tunataka fomu...tunataka kitambulisho”walisikika wananchi  wa buhalahala.

 “Mtu yupo nyumbani amelala anaandikishwa,sisi tuliokuja kukesha hapa tunaambiwa  twende kalangalala wao wamechoka macho yanawauma ,hivi hatima yetu nini na sasa ni saa 3:00 usiku kwanini wasituandikishe  ?hatoki mtu hapa ,kama ni polisi aje tu”alisema Julius Maugo mkazi wa Mwatulole.

Katika kituo cha Kalangalala Sekondari hali nayo ilikuwa tata ambampo mwananchi ilifika eneo hilo majira ya saa 1:30 na kushuhudia wananchi zaidi ya 200 wakiwa kituoni wengine wakipigana ngumi na kusukumana kila mmoja anataka aandikishwe.

“Hapa muda unaisha ,na leo(jana) ndiyo mwisho,hatujui hatima yetu ,wananchi wengi hatujaandikishwa,tumeshaomba tuongezewe mashine lakini hatusikilizwi zaidi tunashuhudia wenye pesa ndiyo wanaandikishwa”alisema alisema Mariana Peter mkazi wa kisesa.

Hata hivyo hali ilikuwa mbaya zaidi ilipofika saa 4:00 usiku ambapo wananchi waliamua kupiga fgari ya serikali mawe na kuvunja.

Hata hivyo kaimu mkurugenzi wa halamshauri ya mji Hellen Kahindi aliamua kuongeza muda wa zoezi hilo kwa kata amabzo hazikukamilika ikiwamo Buhalala ,Kalangalala na Mwatulole na zoezi hilo litaanza kesho  kwa kata zote za mjini kwa muda wa siku saba. 

tumefanikiwa kutuliza vurugu za kufungiwa ndani kwa baadhi ya waandikishaji,licha yakuwa tumepata hasara ya kuvunjwa vioo vya mbele magari ya serikali ,lakini kilio cha wananchi tumekisikia na tatahakikisha wote wanaandikishwa



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment