WAKO WAPI MAPACHA ALBINO WALIOTEKWA MIAKA 8 ILIYOPITA?



Na Jackline Masinde
Geita/Nyang’hwale: Huu nimsiba usiyofutika!!!

Ni maneno ambayo nimeona pengine yanafaa kuelezea tukio la   familia ya Watoto wenye ulemavu wa ngozi, Lemy Juma (12) Zakharia Juma (6) waliotekwa na majambazi miaka nane iliyopita.

Tukio hilo liliacha simanzi isiyofutika kwa familia ya Lemy na Zakharia ambao walitekwa na majambazi nyumbani kwao saa 2:00 usiku 14 Augosti 2007, wakiwa kwenye maandalizi ya chakula cha Jioni,huko kijiji cha Buhalahala kata ya Kalangalala wilaya ya Geita .

Ikiwa bado Taifa linahuzunika juu ya Kifo cha Yohana Bahati(1) mkazi wa kijiji cha ilelema aliyetekwa na majambazi mikononi mwa mama yake kisha kuuawa kikatili kwa kukatwa miguu na mikono yake miwili na kiwiliwili chake kutupwa katika shamba la mahindi huko hifadhi ya Bihalamulo wilayani Chato.

Pia tukio la Mtoto Pendo Emmanuel aliyetekwa na watu wasiyojulikana na kutokomea kusikojulikana ambae hadi leo hajapatikana,mtoto mwingine Baraka cosmas(6) huko wilaya ya Sumbawanga ,ambae alikatwa mkono wake wa kulia na watu wasiyojulikana .

Matukio hayo,yaliamsha hisia za waliowengi,huku wengi wakijiuliza nani anafanya matukio haya,kwanini albino wanatekwa na kuuawa,wanaohusika je wanakamatwa?.

Matukio haya yananikumbusha tukio la kwanza kutokea katika wilaya ya Geita la mtoto Lemy na Zackharia waliotekwa hadi leo  hawajulikani walipo na hakuna mtu yeyeote aliyekamatwa na hakuna juhudi zozote zilizochukuliwa dhidi ya tukio hilo.

Najiuliza sipati jibu,watoto hawa wako wapi mpaka sasa.Je? wako hai,nani alihusika na tukio hilo.Je ?hatua gani zimechukuliwa kuhakikisha watoto hawa wanapatikana?.Je? kwanini sijasikia kelele kama ilivyo kwa tukio la Pendo Yohana na wengine?.

Majibu ya maswali haya yananipa utata ndipo nilipoamua kufatilia mkasa huu mwanzo hadi ulipoishia,hivyo nilifunga safari kwenda nyumbani kwa wazazi wa watoto hawa,nikiamini ndiyo wanaweza kunipa majibu yaliyosahihi.

Ni safari ndefu sana,yenye misukosuko ya ubovu wa barabara,iliyoanza saa 2:48 asubuhi kutoka Geita mjini kuelekea kitongoji cha Nyangombe kijiji cha Nyashilanga Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita ilipo familia hiyo kwasasa.
.

Nilivuka mapori na mapori,nilivuka vichaka vya kutisha,nilivuka mito na milima hatimae niliwasili nyumbani kwa mzee Katemi Shigata babu yake na watoto hao  saa 11:40 jioni.

Hakika nilichoka sana,kwani ilikuwa safari ya kuunga unga kutokana na shida ya usafiri katika wilaya hiyo.Jua nalo lilikuwa linaishilia,giza lilikuwa limeanza kutokea kwa mbali.

Ni familia kubwa yenye watu zaidi ya 40 wanaoishi sehemu mmoja,kwamaana baba na mama, watoto,wajukuu,vitukuu,ndugu na jamaa.

Niliona wakiwa wamekaa katika makundi,wengine walionekana wakikusanya kuni za kukoka moto wa kikome,wengine waliingiza ngombe zizini,wengine walionekana wakipasua kuni.Hakika walikuwa katika maandalizi ya jioni.

Nilikaribishwa na wanafamilia hao ambao walionekana kupigwa na butwaa baada ya kuniona huku wakiwa na shahuku ya kutaka kujua mimi ninani na ninashida gani.

“Karibu dada!(mwandishi)nilipewa kigoda cha kukalia.

Walijawa na hofu kubwa, wengi waliamini ni askari nimekuja kuwakamata.

“Dada wewe ninani,siku hizi tunaogopa tukiona watu tu tunajua ni mapolisi wa serikali wanakamata watu”alisema mmoja wa wananfamilia hao huku akinikagua kwa macho.

Nilijitambulisha kwao,na kuwaeleza kilichonileta,wengi walionekana kutoniamini kabisa na badala yake walinihoji maswali yanayohusu jeshi la polisi.
“Hivi dada (mwandishi) hawa maaskari wanaokamata waganga wakienyeji wanatumia utafiti gani kuwajua kama ndiyo wanasababisha mauaji ya albino,maana wanakamata tu watu hata kama siyo mganga?alihoji Kulwa Shigata mmoja wa wanafamilia hao.

Inanipa kazi ngumu kubadilisha mtazamo wao  kama mimi ni raia mwema kwao,ilinibidi nitumie taaluma yangu kuwaleta kwenye mstari, lakini mwisho walinielewa ndipo niliwaleta kwenye mada iliyonileta kwao.

Niliona walijikusanya ,waliokuwa wamesimama walitafuta mahali pa kukaa,waliokuwa mbali waliitana na kuakaa .

Maskini! Bila kujua nilihamsha uzuni na majonzi upya kwa familia hii,mara wote walionekana kukaa kimya kwa muda wa dakika 2,huku mmoja wa wananfamilia hao  ambae baadae niligundua ni mama mzazi wa watoto hao Mihayo Shigata akishindwa kujizuhia na kuanza kulia.

“Wanangu jamani...,nilikuwa nimesahau....,sijui wako wapi,Lemy na Zackharia mko wapi...?,mliondoka mkiwa wadogo sana sasa hivi mmekuwa wakubwa wanagu”alilia kwa uchungu Mama huyo.

 Ooh Mungu wangu!Baba mzazi Juma Charles  nae anashindwa kujizuhia,yeye analia huku akitupia lawama Jeshi la Polisi .

Polisi!!polisi!! wanajali watu wenye pesa...nakumbuka nilito taarifa polisi wakaniambia nikatafute mwenyewe nikiwapata nitawajulisha,Wanangu mko wapi?”alihoji kwa uchungu.


Ilikuwa ngumu kujizuhia,uchungu wa wazazi hawa ulinifanya pia nidondoshe chozi,lakini nilijikaza na kuanza kuwatuliza wanafamilia hawa.

“Jamani hebu tulieni tumweleze,labda tutasaidiwa kuwapata watoto wetu”alisema Charles.


“Dada umeturudishia majonzi tena,tulishasahau haya mambo,mimi siwezi kueleza vizuri,ongea na baba mzazi wa hawa watoto”alisema Katemi Shigata babu wa watoto hao.
Simulizi inaanza.
Inamchukua muda wa dakika tano akilia,huku baba yake Katemi akimbembeleza asilie,”nyamaza mwanangu wewe ni mtoto wakiume jikaze,umsimulie huyu mwandishi labda tutapata msaada wa kuwapata wajukuu wangu”alimtuliza mwanae.

“Ilikuwa ni mwezi Agosti (alianza kusimulia)mwaka 2007 tarehe sikumbuki majira ya saa 2:00 usiku tukiwa tumekaa nje tukisubiri chakula cha Jioni,ghafla walikuja watu watano wakiwa wamevaa kininja(wamefunika uso wao ) huku wamevalia makoti meusi”Charles.

Charles alieleza  alisikia watu hao wakiwa na mapanga wakiwaambia wachuchumae chini na wajifunike uso wao usionekane huku wakigonganisha panga zao.

Niliogopa sana,kwani vitu hivyo havijawahi kunitokea katika maisha yangu,nimekuwa nikisia tu kwingine”alisema .


“Walituambia tulale kifudifudi na tujifunike nguo,tulitii amri,licha yakuwa mimi sikuwa na nguo ya kujifunika,moja ya jambazi hao alinikanyag kichwani ili nisiweze kunyanyauo uso wangu”alisema.

Alisema walipigwa ovyo ovyo na majambazi hao kwa kutumia bapa za panga,huku wakiwaamuru wasipige kelele.

Sikujua lengo la ujio wao hao majambazi, nikiwa nimekanyagwa kichwa nilijiuliza kimoyomoyo hawa watu wanataka nini,mbona mimi ni mtu maskini sina kitu chochote”alijiuliza baba huyo.

Alisema hakuwaza moyoni kama majambazi hao walikuwa na lengo la kuchukua watoto wake,wazo lake halikuwepo kabisa na kwa kipindi hicho kesi za albino hazikuwepo hivyo hilo lilikuwa tukio la kwanza kutokea kwa wilaya ya Geita.

Wakati nikijiuliza hayo nilisikia wakimlazimisha mke wangu aonyeshe walipo watoto,kwani wakati wanatuvamia watoto walikuwa ndani wamelala wanangu watatu,wawili walikuwa albino na moja hakuwa albino.

“Wewe watoto wako wapi,tuonyeshe watoto wako wapi”aliwanukuu ,walimpiga mke wangu ,ndipo majambazi hayo yaliingia ndani na kuanza kutafuta watoto.



“Waliwachukua watoto wote watatu na kuwalaza kifudifudi,lakini nilisikia mmoja wa majambazi hao akiwaelekeza wenzao kuwa hao wawili wawekeni huku.”alisema .


Wakati wakitupiga vibaya na mapanga yao nilisikia watoto wakikimbia ,ambapo majambazi hao walisema kamata hao watoto wanakimbia’kumbe hiyo ilikuwa ni mchezo tu kusema watoto wanakimbia kumbe ndiyo waliwachukua na kuondoka nao”alisema.

Alisema sikuelewa kitu niliona kama maigizo,baada ya muda niliona kimya na jambazi lililokuwa limeniganyaka liliacha kunikanyaga ila niliona mwanga mkali wa tochi.

Sikutaka kunyanyuka kuona kwani nilihisi bado wapo kumbe walikuwa wameondoka ila waliacha tochi kubwa ikiwaka.

Alisema iliwachukua muda wa nusu saa wakiwa wamelela kifudifudi licha ya ukimya mkubwa kutawala,hakujua kama watoto wamechukuliwa.

“Nilinyanyua kichwa change taratibu nakuangaza kuona kama wameondoka,niliona kweupe tu zaidi ya hiyo tochi na mke wangu na dada yangu niliyekuwa naishi nae wakiwa wamelala”alisimulia baba huyo.

Alisema aliwaamsha na kuanza kupiga kelele,wakiomba msaada,wakati huo hawakuwaza kama watoto wao wamechukuliwa kwani waliamini wapo, labda wamekimbilia nyumba za jirani.

“Walikuja watu wakakusanyika majirani wa karibu,tukaweleza yaliyojiri,tuliamua kulala baada ya kuona kumetulia,na tukauliza walipo watoto tukaambiwa wapo kwa jirani”alisimulia.


“Usiku huo haukuwa na amani tena,ulijawa hofu kubwa,sikulala kabisa usiku huo,asubuhi kulipo kucha tuliwafatilia watoto ,tukampata mmoja Masumbuko Juma(17) ambae hakuwa albino”alieleza.

Alimuuliza mwane waliko wenzake  lakini alijibu kuwa  wakati wanakimbia alikimbia na kaka yake Remi na Zakharia lakini walikamatwa na majambazi hayo yeye akakimbia na kujificha kichakani.

Majibu ya mwanae yalimpa mashaka na kuanza kujiuliza sasa watoto wako wapi,na wakati huo hakuwa na wazo kama walichukuliwa na majambazi hao ila siku zilivyozidi kwenda na matukio ya kuuawa albino ndipo alipoanza kuamini kuwa uwenda wale majambazi ndiyo walichukua watoto wao.

“Nilianza  kuwatafuta watoto hao kwenye nyumba za majirani lakini hatukuwapata”alisema.

Alisema waliamua kutoa taarifa kituo cha Polisi Geita juu ya watoto hao kupotea,Polisi waliwaambia waendelee kutafuta wakiwapata watawajulisha.

“Zilipita siku mbili bila mafanikio,wala kusikia fununu,tulizunguka kila kona ya kijiji na mitaa yote hatukuwapata,tulirudisha taarifa polisi,walikuja eneo la tukio na kufanya uchunguzi kisha kufungua jarada namba GE/IR/2688/2007”alisema.

Waliendelea kutafuta maeneo yote ya Geita,walikuwa waanasikia fununu sehemu fulanani amepatikana albino,wakienda kufatilia wanakuta siyo watoto wao.

"Polisi baada ya kufungua jarada hilo hawakuendelea tena ,walikaa kimya tukaamua kuendelea kutafuta wenyewe lakini mpaka leo hii saa na dakika hii ninayoongea sijui watoto wangu wako hai,nani aliwachukua”alisema.

Anasema wakati huo alijua watoto wake walipotea tu kawaida,lakini kadri siku zilivyozidi matukio hayo yaliongezeka,ambapo baada ya tukio la watoto wake lilifata tukio la Zawadi Magindu mkazi wa kijiji cha Nyamaruru ambae alivamiwa na kukatwa miguu na mkono mmoja .

“Tukio hilo liliniogopesha na kuanza kujiuliza tena ,hueanda na wanangu wameshakatwa viungo ,kwasasbabu siko nao karibu,sijui waliko ,tulianza upya kuwatafuta kwa hofu ya watoto wangu kuuawa lakini bado haikuzaa matunda”alisema .

Alisema walikaa tena wakasikia tukio la albino wengine 6 walikatwa mikono,vidole na wengine kunyolewa nywele zao,matukio hayo pia yalizidi kumuumiza moyo.

Baada ya hapo mpaka sasa hivi nikajua kumbe hata wanangu walikuwa kwenye kundi la maalbino wanaotekwa na kuuawa kisha kuchukuliwa viungo vyao,baada ya matukio haya kuongezeka na kutangazwa kila siku.

Masumbuko asimulia .
Masumbuko ambae kwa wakati huo alikuwa na umri wa miaka  10,anasimulia jinsi majambazi hayo walivyoingia ndani na kuwakuta wamelala.

"Tulikuwa tumelala tukasikia nje kunakelele ,tukastuka mimi na Fikiri na Zakharia,wakati huo Lemy alikuwa nje na mama,ghafla majambazi wawili wakaingia ndani na kumchukua Fikiri ,na Zakharia mimi nikajimbaza nyuma ya mlango”alisema.

Alisema alitoka nje kwa kunyata na kukimbia nyumba ya Jirani yao Bahati India alipofika aliwaambia nyumbani kunamajambazi. 

Nilipowaambia wote tukakimbia kwenda kujificha,na India akakimbia nyumba zingine za jirani kuwaambia ili wapige mwano”alisema
Alisema baada ya hapo hakujua nini kilichoendelea kwani alilala kwa jirani hakurudi nyumbani hadi kesho yake.

Alisema kesho yake asubuhi  alipofika nyumbani kwao alikuta watu wengi.”Baba akaniuliza kaka na mdogo wagu wako wapi? ,nikawambia sijui waliko mimi nilikimbia peke yangu.

Alisema baada ya kueleza hayao alisikia ndugu zake walipotea ,watu wakaanza kuwatafuta lakini hawakuonekana hadi leo.

"Najisikia huzuni sana ,kwani sijui ndugu zangu wako wapi,nani aliwachukua,wapo hai au wamekufa?”alihoji mtoto huyo huku akishindwa kujizuhia na kuangusha machozi.

Mama mzazi wa watoto anena ya moyoni.
Baada ya kuongea na mume wake na mtoto wake ,nilimgeukia mama ambae kiukweli alitia huruma,sikutaka kumuumiza lakini ilinibidi tu nifanye nae mahojiano ili kukamilisha taaluma yangu.

Kinachoniuma dada,(mwandishi) wanawake wenzangu ambao watoto wao wamefanyiwa ukatili wamesaidiwa na serikali,walau hata kupata mwili wa mtoto Yohana Bahati,bora mama huyo hata analiona kaburi la mwane”alilalamika.

“Mimi nilieje?Bora wangewakata hata viungo vyao kama alivyokatwa mtoto Baraka Cosmas(6) na kumwacha “alilia mama huyo.

Mama alieleza hisia zake huku akitokwa na machozi yasiyokauka,kuwa Serikali isaidie kuwatafuta watoto wake ,licha yakuwa hajui kama wako hai.

“Sijui wanangu waliwaua...!sijui walikatwa tu viungo wakawaacha?!,sijui walitupwa maporini kama Yohana wakafia huko, mimi sijui Mungu Wangu!!”alilalamika mama kwa uchungu.

Aliendelea kulalamika mama huyo mwenye nzao 10 huku kati ya hizo nzao tatu ni za watoto wenye albinisim ambao ni Lemy ,Zakharia na Marko Juma(6) ambae kwa sasa analelewa na kituo cha watoto wenye albinism mwanza.

Alisema Lemy ndiye mwanae wa kwanza huku Zakharia ni mtoto wa tatu na Pendo ni mwane wa saba,anasema kwa sasa amebakia na watoto saba ambapo wawili ambao ni Albino walitekwa na majambazi huku mtoto wake mwingine ambae siyo albino alikufa kwa ugonjwa tu wakawaida.

Hakika ni msiba usiyofutika kwa mama huyu na familia nzima ya watoto hawa,huku swali lao kuu likiwa ni wapi walipo watoto wao,nani aliwateka,je wako hai au wamekufa,wamekufa kifo gani,kama wapo hai wanaishi wapi na nani anaishi nao?.
Ndugu na jamaa wanena.

Shigata ni babu wa watoto Zakharia na Lemy ambae aliamua kukusanya watoto wake wote wakike na wakiume na kukaa nao nyumbani kwake.

Alisema baada ya tukio hilo kutokea na matukio hayo yakaendelea kuwepo hapa Geita ,na mwanae tena akazaa mtoto mwenye Albino aliamua kuwaambia waje kuishi kwake kulinda usalama wa mjukuu wake Marko Juma(6).

“ waliondoka Buhalahala mwaka 2009 nakuja kuishi kwangu,lakini baadae tukafanya utaratibu wa kumpeleka mtoto Marko kituo cha watoto wenye albino Mwanza kulinda usalama wake”alieleza Shigata.

Kwilabya Shigata,ni mama mdogo wa watoto hao,anakiri kuwepo kwa tukio hilo,nay eye nimoja wa mashuhuda wakuu watukio.

“Yaani siwezi kuielezea siku hiyo,ndoo gete(hapana kabisa),nilijikojolea siku hiyo mimi na ukubwa wangu niliokuwa nao,sikia kwa mtu mwingine tu”alisema Dada huyo huku akikataa kabisa kuvuta kumbukumbu ya tukio hilo.

Viongozi wa kijiji cha Nyashilanga.
Hakika nilikamilisha mahojiano na wanafamilia hao,licha yakuwa ilikuwa kazi ngumu sana kwangu,na giza nalo lilikuwa limeingia,kwani ilitimia saa 1:30 usiku.

Nilimuita Dereva aliyenibeba ,ili kuanza safari yakurudi makao makuu ya wilaya ya Nyang’hwale,ni umbali mrefu zaidi ya saa moja nanusu kwa usafiri wa pikipiki.

Tayari nilijawa na hofu mimi na dereva aliyenibeba,kwani kijiji cha Nyashilanga kilikuwa na giza nene,na mapori makubwa,lakini tulikaza moyo.

Dakika  10 zilikuwa zimepita kufika makoa makuu ya Kijiji tulikutana na ofisa mtendaji wa kijiji Saidi Ndekwa  senta ya kijiji hicho.Tulitumia dakika 5 kuzungumza nae juu ya familia ya watoto waliotekwa.

“Hilo tukio nililisikia,na familia hiyo tunaifahamu kama viongozi wa kijiji kwamba walikuwa na watoto watatu wenye Albino,wawili walitekwa na majambazi na mmoja alipelekwa mwanza kwaajiri ya usalama”alisema Ndekwa.

Alisema wazazi wa watoto hawa walikuwa wakiishi kijiji cha Buhalalahala kitongoji cha Ishinde,ambako ndiko watoto wao walipotelea ,baadae ndiyo wakaja kuishi hapa kwa mzee Katemi ambae ni  mzee wa kijiji hiki kwani ni watoto wake.

Baada ya maongezi hayo ilikuwa  imetimia saa 1:45 usiku,tuliendelea na safari ya kwenda makao makuu ya wilaya,kwaajiri ya kupunzika.

Ohh! Mungu nimkubwa!nilifika mjini Nyang’hwale saa 2:30 usiku,nikiwa salama.
Mashahidi wa tukio hilo kijiji cha Buhalahala
Asubuhi Safari ya kurudi Geita ilianza saa 12:00 kutokana na uchovu niliokuwa nao,niliamua kupumzika siku mzima.

Kesho yake nilifunga safari kuelekea kitongoji cha Ishinde Kijiji cha Buhalahala kata ya Kalangalala kilometa 10 tu kutoka Geita mjini  ambako tukio la kutekwa watoto hao lilikotokea.Lengo lakuja hapa nikuwatafuta mashahidi walioshuhudia tukio hilo.

Moja kwamoja nafikia ofisi ya Kijiji (ambayo kwasasa ni ofisi ya mtaa), nilikutana na mtendaji wa mtaa huo Mathias Mbassa na kumweleza kilichonileta,alionekana kuwa mgeni wa tukio hilo ndipo alipomtafuta mwenyekiti wa kijijiThomas Mageni.

Mmh!umesema lilitokea lini?hebu ngoja nimpigie Mwenyekiti”alisema huku akichukua simu yake mfukoni (alianza kutafuta namba kwenye simu).

Hallo! Mwenyekiti hebu njoo ofisini hapa mara moja”alikata simu na kunisihi nisubiri dakika chache.

Dakika chache Kadhaa aliwasili Mwenyekiti huyo,alielezwa na mtendaji nilichomweleza kisha kunitambulisha kwake.

“Hilo tukio nalikumbuka kulikuwa na familia mmoja ilikuwa na watoto albino wawili walipotea usiku baada ya kuvamiwa na majambazi na wakati huo mimi nilikuwa mwenyekiti wa kijiji hiki”alisema huku akivuta kumbukumbu.

Ndiyo..nimekumbuka mama,ulikuwa unasemaje sasa?aliniuliza mwenyekiti huyo,nikamweleza yaliyoyangu.

Alisema tukio la kutekwa kwa watoto hao alilipata kesho yake Asubuhi baada ya kupigiwa simu na mwenyekiti wa kitongoji husika.

Nilienda eneo la tukio na kuanza kupiga mwano kuwakusanya wananchi wote,ikabidi tutoe taarifa polisi juu ya watoto kupotea na kuvamiwa na majambazi.

Alisema Polisi ilibidi wamkamate baba mzazi wa watoto hao ,kwa kosa la tukio kutokea usiku na kuamua kulala badala ya kupiga yowe ili watoto watafutwe.

“Baba huyo alikuwa hawezi kujieleza ilibidi akamatwe na polisi kuwa ameuza watoto wake ,kwanini hakupiga yowe usiku huo”alisema na kuongeza baada ya kukamatwa baba huyo muda mfupi tulimuona ameachiwa sisi tukajua labda ameonekana hana hatia”alieleza.

Alisema baada ya hapo sikuona tena chochote na hao watoto hawakuonekana hadi leo.

Baada ya maelezo ya mwenyekiti tulitembea Kilometa 2 kwenda nyumbani ilikokuwa familia hiyo,kweli tulikuta hakuna nyumba watu walishahama,kumegeuka mashamba nasiyo makazi tena.

Zilionekana Nyumba jirani na eneo hilo mita 300,tulienda katika nyumba hizo nakukuta watoto wakicheza,tuliwauliza walipo wakubwa,hawakutuelewa kwani hawakujua Kiswahili.

Wakubwa zenu wako wapi?aliwahuliza mwenyekiti kwa lugha ya kisukuma,walimjibu ‘alemomunumba omayo’(mama yuko ndani),walimuita mama yao.

Mama huyo  ambae alikuwa mrefu na mtu mwenye miraba mine,alitoka nje huku akionekana anafuta machozi kwenye macho yake,hii ilionyesha alikuwa anapika ndani.

Alisalimia,kwa Lugha ya kisukuma,hakika mama alikuwa mchangamfu ajabu,alileta viti tukakaa.

Hakujua Kiswahili hivyo aliongea kisukuma mwanzo mwisho,nilimuuliza juu ya tukio la watoto Albino waliotekwa,alionekana kuwa mwenyeji wa tukio hilo na kusema na lifahamu lakini mimi hapa ni mgeni nilikuja mwaka juzi,labda kwa mzee Bahati India.

Tulikwenda kwa mzee India ambae ndiye Shuhuda namba moja aliyeletewa taarifa na Mtoto Masumbuko muda mfupi tu baada ya majambazi hao kuvamia.

“Hapa anasimulia..”ilikuwa saa 3 hivi,alikuja mtoto anakimbia huku analia,akatuambia nyumbani kwao wamevamiwa na majambazi”alisema.
Alieleza kuwa taarifa hizo ziliwastua familia nzima ,ambapo kila mmoja aliogopa na kukimbia ovyo ili kujificha.

Nilikimbia kwa jirani yangu Edward Kulwa nikamweleza kwa jirani yetu wamevamiwa,tulianza kupiga yowe ili kujikusanya twende eneo la tukio tukiwa wengi”alisema.

Alisema walipofika nyumbani kwa Charles walikuta majambazi wameondoka,wakamwambia mwenye mji wapige kelele ili watu waje mwenye mji akakataa na kuwaambia wakalale kwani majambazi wameshaondoka.

"Tulirudi kulala kila mtu,asubuhi kulipokucha ndipo ikaonekana watoto wawili hawaonekani,tukaaanza kupiga mwano ili kuwatafuta watoto lakini hawakuonekana hadi leo”alisema India.

Uongozi wa walemavu wanena.
Baada ya kujiridhisha na mashuhuda hao,nilimtafuta mwenyekiti wa Chama cha Walemavu mkoa wa Geita Isack Timothy eye alinipa orodha ya matukio ya watu wenye ulemavu wa ngozi waliokwisha kutekwa kujeruhiwa na wengine kuuawa.

"Nakubali kwenye orodha yetu tunao watoto wawiliwa familia moja  ambao walitekwa hadi leo hawajaonekana,tukio hili halikupewa uzito wowote na hata jeshi la polisi halikufatilia hadi leo”alisemaTimoth.

Pia albino watatu kwa wilaya ya Geita,na mmoja kutoka wilaya ya Chato waliuawa kwa kipindi cha mwaka 2008-2015,ambao ni Lwegamoyo Kilanga mkazi wa kijiji cha Chigunga alikatwa mkono,Zawadi Magundu mkazi wa Nyamaruru alikatwa miguu na mkono mmoja na Gaspali Elikana alikatwa mguu wake wa mmoja.

Alisema kuwa waliojeruhiwa mpaka sasa katika wilaya ya GeitaBibiana Mbushi aliyekatwa  mguu wa kulia na vidole  viwilii vya mkono,Nelick Elias(4)mkazi wa kijiji cha Kaseni alinyolewa nywele zote za kichwani kwa ktumia wembe na Adam Robert(12) mkazi wa  nyaruguguna wilaya ya Nyang’whwale  alijeruhiwa mkono wa kushoto na kukatwa vidole vya mkono wa kulia vyote.

Katika matukio yote hayo ,ni tukio moja tu la Zawadi Magindu ambalo watu waliofanya tukio hilo walichukuliwa hatua  5 machi mwaka huu kwa kuhukumiwa kunyongwa na ni baada ya watu kupiga kelele juu ya kifo cha mtoto Yohana Bahati.

Timoth alisema hajalidhika na utendaji wa jeshi la polisi na serikali kwa ujumla katika kufatilia matukio ya kuuawa ,kutekwa na kukatwa viungo kwa Albino.

“nashindwa kuelewa hivi karibuni majambazi yalivamia kituo cha polisi Bukombe,tuliona jinsi serikali na Jeshi la Polisi lilivyofanya kazi hadi majambazi na siraha zilizoporwa kupatikana lakini unapozungumzia albino wanachukulia mambo kilahisi”alisema.

Alisema kwa mantiki hiyo inaoneka thamani ya albino inazidiwa na thamani ya Bunduki.
Jeshi la Polisi linatambua tukio hilo?.

Nilikutana na Kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa Peter Kakamba namtonya juu ya tukio hilo na kutaka kuja kama kuna watu ambao wameshakamtwa au la,lakini anaonekana kutokulifahamu kabisa,ndipo aliponikbidhi kwa Ofisa Upelelezi wa makosa ya jinai mkoa Peter Kayumba.
Ofisa huyo anaomba nimpe muda ili afatilie kujua kama kunatukio la aina hiyo.

“Naomba nifatilie,maana sisi nimgeni ili nijue kama kunatukio la aina hiyo na ikiwezekana niende kwenye hizo familia”alisema Kayumba.

Gerald Ruhele ni Mkurugenzi wa mtandao wa  Mashirika yasiyoyakiserikali yanayotetea haki za binadamu mkoani Geita yeye anasema analifahamu tukio hilo na kwamba walishatoa taarifa kwa vyombo vya dora na serikali hivi karibuni ili kulifatilia.

“Tunafahamu tukio hilo sisi kama mtandao wa mashirika yasiyoyakiserikali na linatuumiza sana,tumeandaa warsha mwezi huu utakao husisha wadau wote na tuki hilo tutalipigia kelele ili waliohusika wachukuliwe hatua”alisema.
Mwisho
 Wananchi mkoa wa Geita wakiwa katika matembezi ya amani ya kupinga mauaji ya Albino yaliyofanyia Februari 27 mwaka huu.











Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment