Jackline
Masinde
Geita:Ilikuwa
ni dakika 45 ya saa 4:00 asubuhi tangu nilipofunga safari kukifikia kijiji cha Nyakabale kilichopo mjini
Geita.
Nikiwa
kijijini hapo, niliona nyumba nyingi
zilizojengwa mithili ya makambi ya wakimbizi ama mahema.
Wakazi wa eneo hilo walionekana wakichapa kazi
haswa.
Magari
yalipishana,pikipiki nazo hazikuwa nyumba ambazo zilionekana zimebeba viroba
vya mawe na abiria wanneau zaidi kwenye
pikipiki moja maarufu kama mishikaki.
Hakika
watu wa kijiji hiki hawakuwa wavivu haslani kwani kila mtu alijishughulisha,si
watoto,si vijana,si wanaume wala wanawake.
Laiti
kama watu wote nchini wangekuwa wanafanya kazi kama wanakijiji hawa hakika
Taifa lingekuwa mbali kimaendeleo.
Walionekana
wakibeba mawe,wengine wakianika udongo,wengine wakiponda mawe,wengine wakifua
dhahabu kwenye makarai na magunia.
“Lete mawe wewe acha kuzubaa,hali ya hewa
inabadilika, mvua muda wowote inanyesha”alisikika kijana mmoja.
Pia
nilishuhudia makundi ya vijana yakiwa yamebeba nyundo,sururu na Moko wengine
walipanda na wengine walishuka toka milimani.
“Hoya
wahi mida ya mafeed kunywa Chai”alisikika mmmoja wa vijana Kijijini hapo.
Kweli
kijiji hiki kilichangamka sana,ukiachilia mbali pilika nilizoziona pia nilisikia kelele za mashine zikisaga mawe.
Ilikuwa
ni kelele ya aina yake ,kusikilizana ilikuwa shida kwangu,lakini wao
walionekana kuzoea hali hiyo.
Ukiachilia
mbali kelele za makarasha pia kulipigwa mziki wa juu kwenye baa zilizopo
kijijini hapo.
Ilikuwa
ni kazi mtindo mmoja lakini na starehe pia kwani wengine walifanya kazi na
wengine walionekana wakinywa pombe asubuhi na mapema.
“Wewe
mama ongeza bia moja,hapa ni starehe na kazi mtindo mmoja ..leta tukushikie
mtoto huyo,mtakujaje na watoto kazini?”alisikika kijana mmoja akimhoji binti wa
miaka 18 aliyekuwa akiwahudumia.
Zaidi
niliona wanawake wengi.Wengine wajawazito,wengine wakinyonyesha watoto na
wengine wakiwa wamepakata watoto wao wachanga migongoni, huku wakigoroga udongo
uliyochanganywa na maji kwa kutumia mikono yao kwenye makarai.
Baadae
niligundua kuwa matope hayo ni udongo unaosadikiwa kuwa na dhahabu,iliyochanganywa
na sumu ya zebaki ,ulikuwa ukisafishwa tayari kwa kupata dhahabu.
Pia
nilishuhudia Watoto wadogo kuanzia 0-5 walikuwa wakicheza chini michezo ya
kitoto.Walijipikilisha kwenye makopo na wengine wakiwaigilizia wanavyofanya
mama zao kwa kukoroga udongo kwenye makopo.
“Nipe
kopo langu...mama niwekee udongo na mimi nikoroge”alisikika mtoto wa umri wa
mika 5 akimweleza mama yake mzazi.
Watoto
wengine walikuwa wakicheza mpira,wengine walikuwa wakichezea maji machafu
ambayo yalionekana yakitililika kutoka kwenye mwalo wa kusafisha dhahabu.
Maji
hayo niyale ambayo tayari yamechanganywa na sumu ya zebaki ambayo nihatari kwa
afya ya mwanadamu.
Aidha
niliona watoto wengine wakikoroga udongo kwenye makarai.Watoto hao walisadikika
kuwa na umri wa miaka 6-15.
Wengine
walikuwa wakizurula ndani ya machimbo hayo wakisubiri kupewa vibarua vya
kusafisha dhahabu,huku wasichana wadogo wengine wakiwa wameketi katika baa
wakisubiri wateja.
Ilinipa
wakati mgumu sana kujua kwanini kijiji hicho kina wanawake wengi na watoto
wadogo ambao wanafanya kazi ya uchimbaji jambo ambalo ni kinyume cha sheria za
nchi na sera ya mtoto
Wakati
nikiwa bado ninatafakari hayo mara nilimuona mama mmoja mwenye miraba
mine,amabye baadae aliniambaia ana umri wa miaka 35.
Mama
huyo ulikuwa akifanya kazi ya kukoroga udongo kwenye makarai aliwakati huo
akiwa amezungukwa na watoto wake wanne.
Nilimsogelea
mama huyo na kuomba kuongea nae ambapo mazungumzo yetu yalianza hivi:
Mwandishi:pole
mama na kazi..
Mama:Asante
mwangu ,karibu(alinikalibisha)
Mwandishi:
Asante mama,kwanza Shikamoo..
Mama
;Marahaba mwanangu.
Niliketi
kwenye ndoo iliyokuwa jirani na mama huyo.
Mwandishi:samahani
mama(nilijitambulisha).
Mama:Nashukuru
kukufahamau mwanngu,wengine sisi tulishazoea shida tu kama unavyotuona
tunahangaika na makarai haya..
Kauli
ya mama huyo ilinivuta na kutaka kufahamu zaidi.
Alijitambulisha
kuwa yeye ni Kabula Satongima (35)ni mama mjane mwenye watoto wanane.
“Nilizaliwa
kijiji cha Bupandwa wilaya ya Sengerema mkoa wa mwanza,ni mtoto wa kwanza kati
ya watoto 15 katika tumbo la mama na
baba yangu”alijitambulisha.
Satongoma alisema kuwa aliolewa akiwa na umri
wa mika 14 huko kijiji cha Nyiboko Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara.
“Niliishi
na mume wangu huko Nyiboko maisha yakawa magumu mwaka 2013 mwazi januari mume
wangu alihamia Geita ikiwa nimoja ya kutafuta maisha”alisema mama huyo.
Satongima
alieleza kuwa aliamua kumfata mume wake
na kuja kuishi nae katika kijiji cha Nyakabale.
Nikiwa
nyakabale nilipata ujauzito wa mtoto wangu wa mwisho,lakini wakati naendelea
kulea mimba yangu mume wangu alikuwa akifanya kazi ya kuokota mawe yanayotupwa
na wazungu”alisimulia.
Alisema
siku moja mume wangu aliondoka nyumbani alfajiri na kwenda msituni kutafuta
mawe,akiwa huko alipigwa risasi na askari wa fanya fujo uone(FFU) akafariki
dunia.
Nililetewa
tu taarifa na wenzake,hivi ninavyoongea hata maiti ya mume wangu sikuiona na
sijui alizikwa wapi”alisema .
Mama
huyo alisema “mama humu unavyotuona wanawake wengi waume zetu wamekufa kwa
kupigwa risasi na askari wanaolinda mgodi”alisema.
Hakika
mama huyu alionekana kutokujua chochote juu ya haki za watoto na ulinzi kwa
mtoto,na wala halionekana kutojua kama kumtumikisha mtoto kazi ni kosa
kisheria.
“Dada
hizo sheria mimi sizijui...sijasoma,ninawatoto wengi wasiponisaidia kazi
tutakula nini?na sinauwezo wakusema niwasomeshe”alilalamika kwa kujitetea.
Nilimuuliza
mama juu ya kazi yake ya kuosha dhahabu kuwa ana muda gani anafanya kazi hiyo
na amenufaika nanini.
“Mama
hii kazi tunafanya tu,lakini hakuna tunachokipata zaidi tunaambulia magonjwa
tu”alisema mama huyo.
Alisema
tangu aanze kufanya hiyo kazi anamiaka minne,zaidi hakuna alichonufaika nacho
juu ya hiyo kazi.
“Hapa
inanisaidia tu kupata pesa za kuhudumia wanagu wapate chakula basi lakini
kusema iniinue kiuchumi hakuna kabisa”alisema.
Alisema
kila siku asubuhi udamka yeye na watoto wake nakwenda kwenye mialo ya kusafisha
dhahabu .
Hii
ndiyo kazi yangu ya kila siku ,nikiamka asubuhi huwa ninawakusanya watoto wangu
weote tunakuja kufanya hii kazi”alisema Satongima.
“Tukifika
hapa huwa tunatafuta vibarua vya kuosha dhahabu mimi na wanangu,nikishapata
huwa nawapangia wanangu karai kila mmoja anatakiwa kuosha karai 4 kwa
siku”alisema.
Alisema
kuwa kila karai moja analipwa sh.250 hivyo kwa siku anaweza kupata sh30,000.
Santongima
aliongea yote hayo huku akiwa amezungukwa na watoto wake wadogo sana kiumri
ambao pia walisafisha dhahabu iliyowekewa sumu ya zebaki.
Huwa
tunakuja na mama anatuambia tuoshe dhahabu ,nasisi tunafanya ili tumsaidie mama
alisema Anna Otieno (8).
Tunafanya
tu,licha yakuwa tunaumia sana kukaa chini muda mrefu,pia baridi kali ikifika
jioni na kichwa kinauma”alisema Otieno.
Lakini
swali je mama huyu na watoto wake wanafahamu madhara ya sumu hiyo?
Mimi
sijui kama inamadhara japo nasikia watu wanasema inamadahara lakini sina jinsi
nikiacha kwa kuhofia madhara nitakula nini na wanangu?alihoji Satongima.
Siyo
mama huyu tu aliyeonekana akifanya kazi hiyo huku akiwa na watoto wake wadogo
,lakini pia nilikutana na mama mwingine.
Naitwa
Savera Jonh (20) ninamiezi sita tangu nianze hii kazi”alisema.
Nilikutana
na Savera akiwa amebeba mtoto wake mchanga mgongoni aliwakati akisafisha
dhahabu.
Alinieleza
huku akiendelea na kazi yake kuwa alipewa mimba na kijna mmoja mchimbaji,lakini
gafla mume wake huyo alipotea,hajui kama yu hai au alishakufa.
Sina
kazi yakunisaidia kupata chakula na mavazi,nalazimika kufanya kazi hii”alisema
Savera huku akiwekewa sumu ya Zebaki kwenye karai alizokuwa akizikoroga.
Wananwake
wengi na watoto wanajihusisha na kazi ya kusafisha dhahabu bila kunzingatia usalama
wao.
Nikiwa
kijijini hapo nakutana na mwanamke mjamzito ambae alikuja kwenye mwalo wa Shija
Boniphace akiomba kibarua cha kusafisha dhahabu.
Kaka
nimekuja leo vipi kazi ipo?alihoji na kujibiwa,”kazi ipo niwewe tu kaaa tukuchanganyie
udongo”alisema .
Boniphace
alichukua udongo unaudhaniwa kuwa na dhahabu kwenye karai kisha kuweka sumu ya
zebaki na majivu.
Pia
aliweka maji ndani ya karai hilo na kumwambia mama huyo mjamzito huku akiwa
amebeba mtoto wake mchanga mgongoni.
“Ninamimba
ya miezi saba, mwanagu ana mwaka mmoja,nafanya vibarua ili nipate ela ya kula
sina mume kama unavyoniona”alisema dada huyo.
Hakika
ni huruma kwa mama huyo ambae alifanya kazi ya hatari huku akiwa amekaa chini
na wakati ni mjamzito na mtoto mgongoni.
Tunaporejea
katika sera ya mtoto ya mwaka 2009 inazungumzia ulinzi wa mtoto kuwa unaanzia
tangu siku ya kwanza mimba inapotungwa,hivyo mama mjamzito haitaji kelele
zozote ,anahitaji utulivu wakutosha ili kulinda usalama wa mtoto..
Lakini
hali iko tofauti kwa mama huyo,ambae anafanya kazi kwenye makelele na sehemu ya
hatari kwa mtoto aliyemgongoni na aliyekotumboni
“Siwezi
kumwacha mtoto nyumbani peke yake nalazimika kuja nae huku kwasababu bado
nimdogo”alisema .
Lakini
mama huyu anafahamu madhara ya sumu hiyo licha yakuwa anaishika na kuitumia
kila siku?
Mimi
sijui kama kuna madhara,ila kila siku jioni huwa nasikia kama moto unawake
kwenye mikono,kichwa kinauma na pia huwa ninababuka ngozi”alisema.
Kwa
mujibu wa daktari wa hospitali ya wilaya ya Geita Adamu Sijaona anabainisha wazi madhara ya sumu
hiyo endapo mtu ataishika kula au kuvuta hewa yake.
“Zebaki
ni sumu hatari sana kwenye mwili wa mwanadamu hasa inapotumika muda mrefu kwa
kuigusa,kula au kunusa”alisema.
Alisema
moja ya madhara makubwa ya sumu hiyo ni kubabuka ngozi,ngozi kupasuka ,ngozi
kuvimba na kutoa magamba,kuharibika kwa ini na inaweza pelekea kifo.
Alisema
sumu huyo inamwingia mtu kupitia damu,ambapo inaenda kuathiri mfumo wa damu.
Lakini
Pamoja na madhara hayo mwananchi ilishuhudia akina mama wajawazito na hata
wanaonyonyesha na watoto wakiishika sumu hiyo bila hata kuwa na vifaa vya
kuzuhia ngozi ya mwili kugusa sumu hiyo.
Watoto
wadogo akiwamo Tereza Jonh (14) na Hapness Deusi (13) walionekana wakimiminiwa
sumu hiyo kwenye karai lililokuwa na udongo unaodhaniwa kuwa na dhahabu,kisha
waliishika sumu hiyo wakati wakichanganya sumu na udongo kwa mikono yao.
Watoto
hawa wanaishi mbali na wazazi wao kwani Tereza wazazi wake wako katoro lakini
yeye yuko Nyakabale kwenye machimbo.
“Huwa
nalala huku kila siku kwa rafiki zangu,asubuhi kukicha tunazunguka kutafuta
vibarua humu machimboni”alisema Tereza.
Anasema
usalama wake ni mdogo sana kwani kunasiku zingine wanabakwa na wachimbaji,siku
zingine wakikosa vibarua wachimbaji wanawaambia wakafanye nao tendo la ngono
ndiyo wawaepe vibarua.
“Niliwahi
kubakwa na mchimbaji,niliomba ela ya kula kwa mchimbaji Yona ,jioni ilipofika
akaniambia nimlipe...nikakataa ndipo aliponibaka mbele ya wenzangu”alisema.
Pia mama mjamzito Naomi Gerald (18) mwenye
ujauzito wa miezi 5 alionekana akimiminiwa sumu hiyo kwenye karai lillilokuwa
na udongo na maji .
Dk Sijaona alibainisha pia madhara ya sumu
hiyo kwa watoto wachanga wanaonyonyeshwa,wanawake wajawazito na watoto wadogo.
Alisema
mtoto mchanga anayenyonyeshwa anapoigusa sumu hiyo,au kuila anaweza kuwa na
midomo myekundu,nywele kunyonyoka,,kudhohofika kwa mwili kupoteza uwezo wa
kuona kwenye mwanga,inaathiri pia ukuaji wa mtoto.
Hii
sumu ni hatari pia kwa watoto wachanga,wanaweza ipata kupitia maziwa ya mama
ambae ameathirika na sumu hiyo,pia mtoto anapoigusa “alisema Sijaona
Alisema
kwa upande wa mama mjamzito,anaweza kuzaa mtoto njiti,kuzaa mtoto akiwa na
upungufu wa uzito,mimba kuharibika,au kuzaa mtoto mwenye kasoro ya viungo vya
mwili.
“mama
anaweza kupata shinikizo la moyo,kupooza ,kupata magonjwa ya figo,kuumwa na
kichwa sana na kuwa na baridi
kali”alisema.
Sofia
Elias ni moja ya wananwake anaeleza kupata madhara ya ngozi ya mwili wake baada
ya kuanza kufanya kazi hiyo alianza kuvimba ngozi yake .
“ilitokea
tu baada ya kufanya kazi hii ya makarai nilianza kuvimba miguu na mikono na
baadae ilianza kubabuka ngozi”alisema.
“Niliacha
kwa muda kazi hiyo hali ikarudi kuwa nzuri,lakini nimelazimka kurudia kazi hii
ili kujikwamua na umskini.
Elina
Masanja nimama mwenye watoto wawili,anaeleza kuwa huwa anakuja na watoto wake
hao kufanya kazi ya kuzungusha.
Mwanangu
kama unavyomuona hali yake ya afya siyo nzuri,huwa anaumwa mara kwa mara,afya
yake nidhohofu sana nywele zake zinakuwa nyekundu”alisema.
Kwa
mujibu wa Dk sijaona anasema kuna kesi mbalimbali za magonjwa yanayoshabiana na
madhara ya sumu hiyo lakini hawana uthibitisho sahii juu ya ugonjwa huo kama
chanzo chake ni sumu ya zebaki.
“Katika
hospitali yetu ya wilaya tunapokea kesi za mimba kuharibika 8,9 hadi 10 kwa
mwezi ,pia wagonjwa wenye matatizo ya ngozi ni 5-6 kwa mwezi huku kwa upande wa
watoto njiti ni 2-3 kwa mwezi”alisema.
Kutokana
na takwimu za Mganga huyo tunaweza sema kwa mwaka zaidi ya mimba
120uharibika,huku watu wenye matatizo ya ngozi ni zaidi ya 36 mwaka.
Lakini
wanaowapa vibarua hawa akina mama na watoto wanasemaje juu ya usalama wao?
Shija
Boniphace ni mmoja wa wamiliki wa mialo machimboni hapo.
Alisema madhara wanayafahamu lakini wengi walikuja wakiliia kufanya hii kazi na hatuwezi kuwazuia.
Wasipofanya kazi watakula nini dada?sisi hapa ni wachimbaji wadogo hatuna uwezo wa kununua vifaa vya kuwapa hawa akina mama na watoto pindi wanapofanya kazi ya kusafisha Dhahabu”alisema mmiliki huyo.
Naamini sheria zinazomlinda mtoto zipo katika ofisi zote hapa nchini,swali langu hizi sheria zimewekwa kama mampambo au la...Pia mkoa wa Geita unamashirika zaidi ya 50 yanajihusisha na mabo ya haki za watoto,lakini suala la ajira hatarishi na usalama wa mtoto bado nikubwa na kila siku kunamashirika yanapewa misaada.
Uongozi
wa kijiji unasemaje?.
0 comments:
Post a Comment